Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Huyu ndie Mwanaume alieacha kazi ili apate muda wa kuhudhuria misiba

Luis Squarisi Mwanaume alieacha kazi ili apate muda wa kuhudhuria misiba

Mon, 2 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Linapozungumziwa suala la uraibu baadhi ya watu hudhani jambo hilo linaishia tu kwenye kunywa pombe, kula, kuvuta sigara au usingizi, lakini ukweli ni kwamba uraibu upo kila mahali na katika vitu mbalimbali.

Ukiachana na hao wenye uraibu wa ulevi au kula, fahamu kuwa yupo mwanaume aliyeathirika na tabia ya kupenda kuudhuria kwenye mazishi, hadi kupelekea aacha kazi apate muda wa kutosha wa kwenda kwenye mazishi.

Mwanaume huyo anafahamika kwa jina la Luis Squarisi kutoka mji wa Batatais, Brazil ambaye anauraibu huo wa kupenda kuhudhuria mazishi.

Inaelezwa kuwa baada ya kifo cha baba yake aliyefariki mwaka 1983, ndipo Luis alijikuta akianza tabia hiyo ya kushangaza.

Na katika ukuaji wake aliendeleza jambo hilo hadi kufikia mbali zaidi kwani amewahi kuweka wazi kuwa aliacha kazi yake ili apate muda mwingi wa kuudhuria kwenye mazishi mbalimbali.

Jambo hilo limekuwa la kawaida na kumpelekea kupata umaarufu kwenye mji wa Batatais, kwani watu wamejikuta hawatamani Luis apate matibabu ya kuondokana na shida hiyo.

Kwani kila afikapo kwenye mazishi wanamuona kama faraja na wakati mwingine asipo onekana watu huuzunika zaidi.

Pia Luis amewahi kukiri kuwa kila siku akiamka anasikiliza redio kujua sehemu zenye msiba, ili aweze kuhudhuria na asiposikia kwenye redio hupiga simu hospitali kwa ajili ya kufahamu watu waliofariki.

Hivyo basi hujikuta akifika katika misiba mbalimbali hata ile ambayo hamfahamu mtu yeyote kwa ajili tu ya kufurahisha nafsi yake, na asipofanya hivyo hata kwa wiki moja tu hujikuta akihisi kuumwa kabisa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live