Menu ›
Burudani
Sun, 25 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kama tunavyojua wapo baadhi ya watu pesa kwao sio kitu, sasa tumeamua kuwasogezea sehemu ambayo wataenda kuenjoy maisha, ambapo ni katika hotel yenye gharama zaidi duniani iliyoko chini ya maji iitwayo ‘The Lover's Deep St. Lucia’.
Hotel hiyo iliyoko chini ya maji katika pwani ya St. Lucia nchini West Indies, inagharimu kiasi cha dola 292,000 ambayo ni zaidi ya tsh 744 milioni kwa usiku mmoja.
Katika hotel hiyo utafanikiwa kuona viumbe mbalimbali vinavyopatikana baharini ukiwa kitandani kwako vilevile pia kuna, baa, choo, na sehemu nyingine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live