Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hizi ndizo Filamu zilizomkosha Obama 2023

Barack Obamas Fav Movies Rais wa Zamani wa Marekani, Barrack Obama

Fri, 29 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kama ilivyo kawaida kwa watu maarufu, mwisho wa mwaka kuachia list ya ngoma, vitabu na filamu zilizowakosha kwa mwaka huo, aliyekuwa Rais wa Marekani Barack Obama ameachia mkeka wa filamu ambazo zimemkosha kwa mwaka 2023.

Obama kupitia ukurasa wake wa Instagram ame-share list hiyo ambayo imeambatana na ujumbe usemao licha ya waandishi na waigizaji kugoma kuleta filamu kali lakini zipo ambazo zimefanya vizuri kwake zikiwemo ‘Rustin’, ‘American Symphony’, ‘Leave the World Behind’ na nyinginezo.

Kwa wiki hii #Obama ameachia list mbili moja ikiwa ya vitabu ambavyo vimemkosha kwa mwaka 2023 vikiwemo ‘The heaven & earth grocery store’ cha James Mcbride, ‘Chip War’ cha Chris Milley na vinginevyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live