Kwa mashabiki wa Diamond Platnumz hakika wanamkumbuka vyema bodigadi wake aliyejibebea umaarufu mkubwa, Mwarabu Figther ambaye kwa muda mrefu wamemwagana na kila mtu anaendelea kivyake.
Sasa Mwarabu amepatikana kupitia wanahabari ambao walitaka kujua kama ikitokea Diamond ametaka wafanye tena kazi pamoja je yupo tayari? Haya hapa ndio majibu yake;
"Mimi sasa hivi nafanya kazi chini ya kampuni. Nina kampuni ambayo ina mabaunsa so naweza kumpatia mabaunsa wa kampuni yangu sababu nafanya kazi na watu wengi japo pia wapo baadhi ambao wanahitaji kufanya kazi na mimi binafsi huwana nakwenda," alisema Mwarabu.