Kwa mara ya kwanza msanii @officialnandy The African Princess ameshea picha ikimuonesha akiwa na ujauzito wa mpenzi wake @billnass ambapo wanatarajia kupata mtoto wa kiume.
Taarifa za Nandy kuwa na ujauzito zilikuwa za muda mrefu lakini bado hazikudhibitishwa na yeye mwenyewe tofauti na ilivyokuwa inadaiwa.
Ikumbukwe kuwa, wawili hao wanatarajia kufunga ndoa mwezi huu wa saba baada ya Billnass kumvisha pete ya Uchumba Nandy siku ya Februari 20 mwaka huu.
Nandy kupitia ukurasa wake wa Instagram ameposti video ya ujauzito wwke akiwa na Billnass kisha kusindikiza kwa maneno haya; "Asante Mungu kwa zawadi hii."