Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Haromize amuelezea Killy

F1d877c63d283308831340d07d2eba84 Haromize amuelezea Killy

Sat, 5 Jun 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MWANAMUZIKI wa muziki wa kizazi kipya, Rajabu Abdul ‘Harmonize’ amesema ilimchukua mwaka mmoja tangu alipopewa nafasi ya kumsimamia mwanamuziki Killy ambaye alitoka King Music.

Akizungumzia juu ya mwanamuziki huyo ambaye kwa sasa ametoa wimbo wake wa kwanza katika lebo ya Konde, alisema ilikuwa changamoto sana kutafuta kitu ambacho anakitaka katika muziki wake.

Alisema anaamini kila msimamizi anakuwa na mfumo wake wa kusimamia wasanii, huku akiamini msanii huyo anaweza kuleta chachu katika tasnia ya muziki Tanzania.

“Mungu kwa kutupa moyo wa subira pande zote mbili na uvumilivu yamesemwa mengi yakukatisha tamaa sijuwi kakusanya watoto wa watu na kupiga nao picha, “alisema.

Chanzo: www.habarileo.co.tz