Menu ›
Burudani
Sun, 7 Mar 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
KUELEKEA Siku ya Wanawake Duniani, msanii Rajabu Abdul ‘Harmonize’ amewausia watoto wa kike kuwa na maamuzi sahihi kwa wanachotaka kufanya kwenye maisha yao.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Harmonize alisema akiona mtoto wa kike anakosea anahisi kama mwanaye Zulekha ndiyo kakosea na kuwaasa hakuna kitu kipya kwenye dunia.
"Mtoto wa kike yeyote anatakiwa ajue yeye ana maamuzi ya kuchagua kutaka kuwa nani lakini hakuna kitu kipya kwenye hii dunia bibi yako, mama, dada na shangazi vyote walishafanya hivyo ni bora kuwa makini na kufanya vitu kwa wakati sahihi," alisema Harmonize.
Chanzo: www.habarileo.co.tz