Prezidaa wa Konde Gang, Rajabu Abdul 'Harmonize' ametoa yaliyopo moyoni mwake kwa kusema kumpata muigizaji Kajala Masanja katika maisha yake ni kama ndoto aliyoota na kutokea kweli.
Harmonize amefunguka hayo kupitia Insta Story yake ambapo ameandika ujumbe huo kwa kuanza kumtaja Mungu.
"Dear God I Know I'm asking for more everyday please just keep giving me what I deserve. Toka life la kwenda mtoni kuteka maji na dumu kichwani kwa mguu ukifika unafua nguo unazianika unazuga na kichupi cha Taiwani mpaka zikauke ndio urudi na Maji home.
Now on tope of the game hata yule dada tuliekuwa tunalipa shilingi 100 bandani na masela kumuona siku ikija TV kijijini kwetu now tunaamka wote and she call me dady! God duwa langu leo liende kwa wasionacho kabisa," alimaliza Harmonize kwa kuweka emoji ya kushukuru.