Staa wa Bongofleva toka Konde Music, Harmonize ameibua mapya kwa kueleza kuwa hajaonja matunda ya mziki wake kwa zaidi miaka 7 iliyopita na hajui ni nani anayechukua pesa hizo kupitia Digital Platform.
Kupitia Instagram ameandika;
Namiliki master zote lakini sijui nani anakusanya pesa zangu, nataka kuwakumbusha kitu nipo hapa kwa ajili ya future yangu, nahitaji maisha mazuri kufanya kazi kwa bidii. Masimango, Manyanyaso, Mateso na kudhalilishwa halafu kuna mtu anachukua pesa zangu kama hivi.
Naacha basi mziki wenyewe mfurahi, nina uhakika hakuna Producer yeyote anayepata haki za uchapishaji wa kazi zake za kuproduce na composer na lawama zote zinaenda kwa wasanii. Ni muda wa kuacha sasa msitumie madhaifu ya watu kujinufaisha.