Msanii Harmonize amemuangukia Naibu Waziri mpya wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma 'MwanaFA' akimuomba aanze kazi kwa kumsaidia kupata malipo yake kutokana na mauzo ya muziki wake kutoka kwa wale ambao anadai ni wasambazaji wa kazi zake Zikii na WCB ambapo anadai hajapokea hata Tsh 100 kwa miaka zaidi ya saba.
Pia amewataka akina Baba Levo, Mwijaku, H. Baba na Diva The Boss, kuacha kubeza juhudi anazozifanya za kupambania haki yake kwani aliwahi kuwasaidia kwa namna moja ama nyingine.
Aidha, amewataka wasambaziji wapya wa kazi zake kujitokeza mara moja ili aweze kuanza kufanya nao kazi.