Menu ›
Burudani
Tue, 20 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rajabu Abdul ‘Harmonize’ amezidi kumfanyia kufuru mpenzi wake, Kajala Masanja baada ya kumzawadia simu aina ya iPhone 14, moja kati ya simu mpya na kali.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kajala ameposti kupitia (Instastory) kipande cha video kinachoonesha simu hiyo na kusindikiza na ujumbe uliosomeka hivi:
"Hommie Wangu Katisha."
Hii sio mara ya kwanza kwa Harmonize kupasuka kwa Kajala. Alishampa ndinga mbili aina ya Range ambazo amezipa namba; Kajala 1 na Kajala 2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live