Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Harmonize ammwagia sifa Paula

Paula Harmonize Harmonize ammwagia sifa Paula

Tue, 27 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Harmonize ni baba wa kambo mwenye furaha na Faraja kubwa kwa mwanawe, binti Paula Kajala, ambaye kwa hesabu ya haraka tu ni kama ameachana na babake wa kambo kwa miaka chini ya kumi.

Juzi binti huyo aliwasifia sana Harmonize na mamake Kajala Masanja baada ya wachumba hao kupakia klipu kwenye Instagram wakicheza ngoma zao mpya za Amelowa na Nitaubeba.

Katika ujumbe huo, ambao ni kwa mara ya kwanza alionekana akimkubali Harmonize kama baba yake, Paula aliwasifia kwa kusema kwamba wanajua kudensi mpaka basi.

Itakumbukwa wawili hao kwa maana ya Harmonize na Paula walikuwa hawaelewana baada ya habari kuvuja mwaka jana kwamba Harmonize alikuwa anamvizia hali ya kuwa alikuwa pia katika mahusiano na mamake, Kajala.

Sakata hilo lilizua chuki katika makundi mawili, Harmonize akakosana na Kajala na pia msanii mwenzake Rayvanny ambaye ndiye alikuwa katika mahusiano na binti huyo kipindi hicho.

Mwaka huu baada ya Harmonize kujitutumua kwa kila namna kuweka mambo wazi baina yake na Kajala, walirudiana na kuvishana pete za harusi, jambo ambalo huenda ndilo pia limepiga pasi hata tofauti kati ya bintiye na Harmonize.

Msanii Harmonize sasa amekuwa akimmiminia sifa kocho bintiye wa kupanga Paula kwenye mitandao huku akisema kwamba anamuonea Fahari kama Tajiri mdogo baada ya kufungua duka lake la kuuza nguo.

“Yaani nakuonea Fahari sana @therealpaulahkajala, Tajiri mdogo Oyaaa. Nani anaweza kufanya Bora kuliko Binti yangu,” Harmonize aliandika kwenye video yenye huyo binti alifanya na kuipakia kwenye Instagram.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live