Menu ›
Burudani
Mon, 6 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tembo KondeBoy "Harmonize" bado ameendelea kumkalia kooni aliyekuwa Boss wake Diamond Platnumz na safari hii amekataa ushindi wa mezani ambao Diamond Platnumz aliamua kumpa kutokana na kutotaka kurushiana nae maneno kwenye mitandao.
Harmonize amekuja kivingine na kueleza jinsi ambavyo DiamondPlatnumz anambania kwenye shows mbalimbali za Kimataifa kwa kusema kuwa Diamond anawaambia waandaaji asipangwe na Harmonize kwakuwa wataonekana wapo levo moja kwenye muziki.
Harmonize ameongeza kwa kusema kuwa kuna wakati Diamond hupiga show za Bure ili tu aonekane amepanda kwenye majukwaa makubwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live