Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Harmonize afutiwa nyimbo YouTube mara ya 3, Uongozi wake

Harmonize+pic Harmonize afutiwa nyimbo YouTube mara ya 3, Uongozi wake

Mon, 27 Jul 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Msanii anayefanya vizuri kwa sasa katika muziki wa Bongo Fleva, Rajab Abdul maarufu Harmonize kwa mara ya tatu sasa ameendelea kufutiwa nyimbo kwenye mtandao wa YouTube kutokana kile kinachoelezwa na kuiga biti.

Hii ni baada ya jana Jumapili Julai 26, 2020 msanii Rosaree kuripoti kwenye mtandao wa YouTube kuhusu kuibiwa biti la wimbo Kanyor Aleng aliouachia wiki mbili zilizopita ambapo Harmonize ameutumia kuimba wimbo wa Amen.

Wimbo wa Amen Harmonize ameuachia juzi kwa ajili ya kuombeleza kifo cha aliyekuwa Rais Awamu ya Tatu,Benjamin Mkapa.

Hii sio mara ya kwanza kwa msanii huyo nyimbo zake kushushwa katika mtandao huo, kwani Novemba mwaka 2019 aliibua gumzo baada ya wimbo wa ‘Uno’ alioutoa kwa mara ya kwanza tangu aachane na WCB kufutwa.

Hii ni baada ya mtayarishaji wa sauti ya wimbo huo, Magix Enga,kutoka nchini Kenya kumpa wiki moja bosi huyo wa lebo ya Konde Gang kuoondoa wimbo huo kabla hajachukua hatua zaidi kutokana na kuchukua biti bila idhini yake.

Hata hivyo baadaye waliyamaliza na wimbo huo kurejeshwa.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz