/>
Muimbaji huyo kutokea WCB amesema kolabo na rapper huyo ni katika maandalizi ya albamu yake na kukuza muziki wa Bongo Flava.
“Am working on my albamu ambayo itakuwa na wasanii tofauti tofauti kwa sababu lengo langu ni tukijiaminisha tunaweza kufanya muziki wetu wa Bongo Flava, ukawa muziki wa Afrika,” amesema.
“Kwa hiyo najitahidi kutoka kufanya kazi na wasanii mbalimbali kuona ni kiasi gani muziki wetu unaweza kuwa wa Afrika, hilo ndio lengo langu,” Harmonize ameiambia Bongo5.
Utakumbuka kuwa mwanzoni mwa March, 2018, Diamond Platnumz ndiye aliyeweka wazi kuwa kuna kolabo kati ya Harmonize na Tyga inakuja.