Menu ›
Burudani
Sat, 2 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Harmonize au Konde Boy; ni staa wa Bongo Fleva ambaye anasemekana ameacha pombe na bangi baada ya kumchumbia muigizaji Kajala Masanja au Mama Pau.
Mtangazaji anayejiita DC wa Insta, Mwijaku ametoa habari ya ndani kabisa kuwa, Harmonize sasa hivi amebadilika kabisa na kazi hiyo imefanywa na Kajala ndani ya muda mfupi tu.
Mwijaku anasema; “Ninyi mnafikiri Harmonize amebadilika ni kazi ya nani? Ni kazi ya Kajala, wewe ulitegemea kama Harmonize hatakunywa pombe? Hanywi pombe siku hizi, havuti bangi, sasa hivi ni mwendo wa maji na juisi kwa hiyo tumpongeze Kajala…”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live