Menu ›
Burudani
Tue, 31 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa Konde Music, Harmonize amesema fedha anazotumiwa kuwanunulia magari wapenzi wake hadi ya zaidi ya Tsh20 milioni, ni zile zake za kunywa bia.
Harmonize amesema fedha hizo hazihusiani na mapato ya Lebo yake ya Konde Music Worldwide.
Kauli yake inakuja baada ya kuulizwa kwa nini anaohonga magari ya thamani kubwa wakati lebo yake wasanii wake hawatoi kazi kwa wakati.
Ikumbukwe kuwa, Harmonize amewahi kumhonga aliyekuwa mpenzi wake, Kajala Masanja magari mawili aina ya range Rover yenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 360 kila moja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live