Menu ›
Burudani
Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Harmonize anasema acheni kujificha, jitokezeni na mlitaje Jina lake kwenye orodha ya vinara wanaofanya vizuri kwenye muziki kwa sasa nchini.
Kupitia insta story yake jana amejifananisha na marehemu Kanumba, Mwigizaji aliyeacha alama kwenye tasnia ya filamu nchini.
“Hivyo kama nikifa leo, kila mmoja atazungumza kuhusu mimi kama ambavyo wanazungumza kuhusu Kanumba. Nipe heshima yangu.
"Nataka nione upendo wenu, acha kuficha ficha ukweli, hakuna anayeweza kufanya kwenye uwezo huu.” ameandika Harmonize.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live