TAARIFA njema ya burudani ikufikiea popote ulipo, Mwanachama wa Chama Kikuu cha Burudani Tanzania, supastaa wa Muziki wa Bongo Fleva, Harmonize ameitangaza rasmi siku ya Machi 5, 2022, kuwa ndio siku rasmi ya tamasha lake kubwa la 'Afro East Carnival' litakalofanyikia jijini Dar es Saalam.
Kulingana na taarifa ya Harmonize kupitia mitandao yake ya Kijamii, tamasha hilo litawakutanisha wasanii mbalimbali kutoka katika nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki, watakaojumuika kwa pamoja kutoa burudani kwa mashabiki wao.
"Hii inakwenda kuwa habari kubwa, wasanii wote wakubwa wa Afrika mashariki kwenye jukwaa moja, nashindwa kusubiri, ninashauku ya kujumuika na kaka na dada zangu 2/03/2022 jijini Dar es salaam," ameandika Harmonize.