Menu ›
Burudani
Wed, 26 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshiriki wa Shindano la BSS, Hamisi BSS amesema hana na hajawahi kuwa na bifu na staa wa Bongo Fleva Harmonize.
Akizungumza na Rick Media hivi karibuni, Hamisi alisema, watu wanaweza tu kuzungumza jambo kulingana na mawazo yao lakini ukweli hajawahi kuwa na tatizo lolote na Harmonize.
"Yule ni kaka yangu, amenitangulia kwenye muziki. Ni mtu ambaye namtazama anisaidie, kwa nanma yoyote ile si tu kunisaini Konde Gang bali hata kwa ushauri na mambo mbalimbali ya kunisogeza mbele kimuziki," alisema Hamisi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live