Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hamisa Mobetto na Tunda wachongewa na Gigy Money Basata

Wed, 31 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Gigy Money ameonyesha kutokubaliana na utaratibu wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) uliowataka ma-video vixen kujisajili katika Baraza hilo.



Tunda, Gigy na Hamisa

Muimbaji huyo ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa Basata walimueleza hilo lakini anaona kuna ma-video vixen wengi ambao hawajasalijiwa na wanafanya kazi hiyo.

“Waliniambia hivyo, lakini sasa Hamisa Mobetto anafanya nini, Tunda tuseme anafanya nini, officialnai anafanya nini, ma-video vixen unataka kuniambia wanajulikana Basata, why Gigy kwa sababu umeonekana ashapata chochote kitu,” amesema Gigy Money.

“Basata mtajalije utamaduni wa msanii mkiwa hamjali Ugali wake, haujali mfuko wake, wewe unaniona tu napendeza unajua mimi napoteza shilingi ngapi,”

Gigy Money kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Mimina baada ya kutamba na ngoma ‘Papa’.

Chanzo: bongo5.com