Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Guiness yaikubali rekodi ya mpishi huyu

Hilda Baci: Mpishi Wa Nigeria Anayepania Kuvunja Rekodi Ya Dunia Hilda Baci

Thu, 15 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mpishi wa Nigeria ambaye amekuwa maarufu nchini baada ya kupika bila kukoma kwa zaidi ya saa 93 amethibitishwa kuwa mshikilizi mpya wa rekodi ya dunia.

Wanasiasa na watu mashuhuri walimshangilia Hilda Baci jikoni kwake huko Lagos wakati wa kipindi cha siku nne mwezi uliopita.

Alitumia zaidi ya sahani 100 katika mchakato huo na aliruhusiwa tu kuchukua mapumziko ya dakika tano kila saa.

Baci amemshinda mshikilizi wa zamani wa rekodi Lata Tondon wa India, ambaye alisimamia muda wa saa 87 dakika 45 mwaka wa 2019.

The Guinness Book of World Records, ambao walilitoa uamuzi wa shindano la kupikia za Baci, wameshiriki video hii wakimpongeza:

"Baada ya kupitia video zote na kufanya tafiti zetu kisha kujiridhisha, tunachukua fursa hii kumtangaza Hilda Baci kuwa ndiye mtu aliyetumia muda mrefu zaidi katika kupika," imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live