Menu ›
Burudani
Thu, 18 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Wakati wapenda burudani wakijiandaa kusheherekea mafanikio ya muziki kupitia tamasha kubwa Afrika Mashariki la Sauti za Busara ifikapo Febuari 9 hadi 12 mwaka huu, waandaji wa tamasha hilo wamebainisha jumla ya wanamuziki 460 wanatarajiwa kushambulia jukwaa hilo katika eneo la Ngome Kongwe, Mji Mkongwe kisiwani Zanzibar.
Baadhi ya wasanii hao ni Grace Matata, Saida Karoli, Segere Originaal, Msafiri Zawose, Jagwa Music, Leo Mkanyia, Tausi Women’s Taarab, Maulidi ya Homu ya Mtendeni na wengineo.
Baadhi ya picha za watumbuizaji wa Sauti za Busara 2018.
Chanzo: bongo5.com