Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gigy Money aachiwa huru

Untitled 1 Gigy Money aachiwa huru

Tue, 15 Jun 2021 Chanzo: eatv.tv

Msanii wa Bongo Fleva, Gigy Money amesema sasa yupo huru baada ya kumaliza adhabu yake aliyopewa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) ya kutojihusisha na sanaa ndani na nje ya nchi kwa kukiuka maadili ya kazi za sanaa.

Submitted by Telesphory on Jumatatu , 14th Jun , 2021 Picha ya Msanii Gigy Money

Gigy amethibitisha hilo kupitia instagram yake kwa kuandika ‘’tumefunguliwa’’ baada ya BASATA Januari 5, mwaka huu kupitia kwa Kaimu Katibu Mtendaji wa baraza, Matiko Mniko,kutangaza kumfungia kutojihusisha na shughuli za Sanaa baada ya msanii Gigy kutumbuiza jukwaani akiwa amevalia nguo zilizodhalilisha utu wake na kubugudhi hadhira ya wapenda sanaa.

Tukio hilo lilitokea akiwa katika tamasha la muziki huko jijini Dodoma katika uwanja wa Jamhuri.

Chanzo: eatv.tv