Msanii mwenye hekaheka zake mjini asiyeishiwa vibwanga Gift Stanford ‘Gigy Money’ amefunguka kuwa kwa sasa yupo single hivyo jimbo liko wazi.
Akizungumza hivi karibuni Gigy amesema hapendi kuficha mambo ndiyo maana ameamua kuweka wazi u-single wake bila kuhofia chochote.
“Jamani eeh mimi nipo single na jimbo lipo wazi natangaza kabisa mimi nipo wazi kabisa na maisha yangu siyo mtu wa kuwa kimya likinitokea jambo ni mwepesi wa kuongea,” alisema Gigy.
Haya atakaye na aende kwa mwanadada huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja na kwa tangazo lake baba wa mtoto kashasepa mazima na mama yuko mpweke biridi inamsumbua.