Menu ›
Burudani
Mon, 25 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii Gigy Money ame-share na sisi kiwango cha pesa ambacho amelipwa na msanii Harmonize kwa kutokea kwenye video ya wimbo wa Dharau ambao amefanya na Ibraah wa Konde.
Gigy amesema alilipwa shilingi Miliono 5 ingawa yeye alitaka 10.
"Harmonize ni rafiki yangu, alinicheki nikamwambia kwamba anipe Milioni kumi lakini akaniambia Gigy kwa video gani basi unatokea kidogo tu basi nikakubali milioni tano,"a alisema Gigy.
Kwenye video hiyo, Gigy ameonekana akimfokea kinyama Harmonize jambo ambalo mwenyewe anasema ndivyo ilivyokuwa inatakiwa na yeye kaitendea haki video.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live