Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Gift Stanford 'Gigy Money' amefunguka kuwa alishawahi kutakwa kimapenzi na mpenzi wa Soshalaiti Nai na alimpa Shilingi Milioni 5 ambazo hakuzikubali.
Gigy ameyasema hayo juzikati kwenye kipindi cha Refresh ya Wasafi TV ambapoeleza:
"Nai ulisikiaga tu nimetoka na Moni Centrozone ukachanganyikiwa sasa hujui sasaivi nitafanya nini naongea mara ya mwisho.
"Huyo mwanaume ulio naye sasaivi unaeona kakubadilishia maisha mimi ameshanifuata na Milioni 5 nikamkataa sijui una mabwana wangapi ila kama mimi napenda vitu vya bure kaa na bwana wako umuulize usitake na mashahidi ninamuheshimu tu ningemtaja jina," alisema Gigy.