Msanii Wa Bongo Fleva, Foby amemuomba mwanamitindo na staa wa Bongo Fleva, Hamisa Mobetto kumu-unBlock katika mtandao wa Instagram na wamaliza tofauti zao.
Kupitia Ukurasa wake Wa IG Foby ameandika:
"Mobetto Unblock Me pls, 3 yrs now picha zako kali ambazo nilikuwa naanza kuziona sasa hivi naziona kwenye pages za watu, nimemiss comments na likes zako pia, embu tumalize haya ni ya dunia mama, hakuna mtu alikuwa anakupenda na kukutakia mafanikio kama mimi na unajua. Wewe ni Madam Hero, Let's end up this pls."
Kwa kauli hiyo inaonekana wawili hao walikuwa kwenye mahusiano mzuri kabla na sasa kuna kidudu mtu kaingia.