Menu ›
Burudani
Mon, 22 Mar 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
MSANII wa Bongo Fleva, Foby ameibuka na kibao cha kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.
Magufuli alifariki dunia Machi 17 na taarifa za kifo hicho zilitangazwa na aliyekuwa Makamu wake, Mama Samia Suluhu, ambaye sasa ndiye Rais wa Tanzania.
Foby anaungana na wasanii wengine kibao kuomboleza kifo cha Magufuli kwa kutunga nyimbo mbalimbali za audio na kutoa video, ambazo zinachezwa katika vituo mbalimbali vya radio na TV.
Kwa mujibu wa Millardayo, Foby ameingia studio na kuimba wimbo wa kumuaga Magufuli akisema ‘Nenda Baba, njia yetu ni moja ipo siku tutakutana’.
Chanzo: www.habarileo.co.tz