Mkali wa muziki wa hip hop Bongo, Fid Q ametoa somo kwa wasanii namna ya kujiweka mbali na msongo wa mawazo (stress) kutokana na kuyumba kwa uchumi.
Rapper huyo ameiambia Dj Show ya Radio One kuwa wasanii wanatakiwa kuwa wabunifu katika kazi zao na kuwa na njia tofauti tofauti za kuwaingizia kupato.
“Katika suala la ubunifu inakupa nafasi kubwa sana kwa sababu unakuwa na akili iliyotulia ambayo haipelekwi pelekwi na stress ndogo ndogo kama za kukosa show za hapa na pale, ni kitu poa na kinapaswa kufuatwa na kila msanii,” amesema Fid Q.
“Pia kuhakikisha anakuwa na njia zaidi ya moja ya kujiingizia kipato yaani mbali na muziki awe na vitu vingine ambayo vitamsaidia kujiingizia kipato,” amesisitiza Fid Q.
Fid Q kwa sasa anafanya vizuri na remix ya ngoma Fresh aliyowashirikisha Diamond na Rayvanny.