Fat Joe alikuwa ni mgeni katika kipindi cha Ebro kwenye Beats 1 ambacho ni kituo cha redio cha muziki kinachomilikiwa na kuendeshwa na Apple Inc.
Katika kipindi hiko Fat Joe alizungumzia wasanii wa sasa wanavyoiga mwenendo wa Lil Wayne.
Joe alisema kwamba “vijana wa sasa ambao wanafanya muziki wa hip-hop wengi wao wanatumia mtiririko wa Lil Wayne.”
Fat Joe kisha aliendelea kusema mawazo yake juu ya Lil Uzi Vert ambaye amepata mafanikio ya kimuziki hivi karibuni. Joe alisema kwamba “Lil Uzi ni toleo baya la Lil Wayne na hafanyi vizuri kama Lil Wayne.”
Lil Uzi alijibu kwa kutweet hivi
Bad version