Penzi limekolewa! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mrembo Fahyma kumfanyia kufuru mpenzi wake Rayvanny kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa usiku wa kuamkia leo Agosti 23, 2023.
Rayvanny alitimiza miaka kadhaa jana Agosti 22,2023 ambapo, awali Fahyma aliandika bonge la ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram kumtakia kila lakheri baba watoto wake huyo.
Ulipofika usiku sasa, wawili hao wakiwa kwenye halfa ya kusherehekea siku hiyo, Fahyma aliomba nafasi ya kutoa zawadi kwa mpenzi wake huyo na ndipo alipomwagia dola ambazo kwa haraka haraka, zinazidi dola 1000 hivyo si chini ya shilingi Mil. 2,505,000.