Mwanamitindo Fahyma maarufu kama Fayvanny amefunguka kuhusu tetesi za ugomvi wake yeye na aliyekuwa mpenzi wa mzazi mwenzake, Rayvanny aitwaye Paula Kajala.
"Mimi sijawahi kujibizana na mtu yoyote yule au nyie mliwashawahi kuona mimi namjibu mtu yoyote yule. Ninachokijua mimi sijawahi kuwa na msongo wa mawazo kwa sababu ya mapenzi na wala sijawahi kuumizwa na mapenzi.
"Sijawahi kuwa na ugomvi na Rayvanny sijui ni kipindi gani tulikuwa na ugomvi, labda nilikufa nimerudi sasa sikumbuki kabisa. Umaarufu wa Rayvanny mimi haunisumbui sababu najua ananipenda mimi sana kuliko mtu yoyote," lisema Fahyma.