Picha ya Mmasai inayoonekana kwenye logo ya chapa ya Jux, African Boy ambayo amekuwa akitumia kwenye muziki na biashara yake ya mavazi, ni ya raia wa Ghana na Jux aliinunua kwenye mtandao wa kuuza picha na kuwa na hakimiliki nayo.
Picha ya Mmasai inayoonekana kwenye logo ya chapa ya Jux, African Boy ambayo amekuwa akitumia kwenye muziki na biashara yake ya mavazi, ni ya raia wa Ghana na Jux aliinunua kwenye mtandao wa kuuza picha na kuwa na hakimiliki nayo. Katika mahojiano na Podcast ya Lil Ommy, Jux alisema awali alitaka kutumia picha ya Simba ila akaona ya Mmasai ni kitu ambacho kinaweza kumtambulisha popote duniani kuwa anatokea ukanda wa Afrika Mashariki.