Picha zinaongea, picha zinaishi picha zinatoa ujumbe maalum usioonekana kwa macho ya kawaida mpaka wakati ufike.
Ukipata muda chukua album yako ya picha pitia picha za zamani ulizopiga na marafiki ndugu,jamaa na hata watu usiowafahamu.Angalia mpangilio wa jinsi watu walivyosimama au kukaa ,angalia mpangilio wa rangi au mavazi ,angalia body language.
Kwa mshangao wa ajabu utakuta kwenye picha fulani watu fulani waliosimama pamoja siku hiyo au kuchuchumaa au kuvaa nguo za aina moja nk.
- wote wamekufa - wote ni matajiri - wote wameoa/wameolewa nyumba moja - wote tabia zao zinafanana - wote ni marafiki wa Damu -wote hivi sasa ni maadui
Tunapojipanga tupige piga na kubadili badili mikao na nafasi si kwa akili zetu bali kuna nguvu nje ya ufahamu wetu nguvu ya kiroho ndio inafanya kazi
Ni nguvu hiyo inayoamua;
Usimame wapi na kwa nini? Ukae wapi na kwa nini? Ufuatane na nani na kwa nini? Umtazame nani na kwa nini?
Ukipata muda pitia picha zako za zamani kisha utagundua kitu.