Msanii Burna Boy (31) Kutoka Nchini Nigeria amekiri kuwa na tatizo la kutosimamisha!
Superstar huyo Wanigeria amekiri hilo kufuatia ex wake mwanadada Stefflon Don (30) kuweka wazi sababu ya kuachana kwao.
Mrembo huyo mwanamuziki wa Uingereza amesema kwa miaka mitatu waliyokuwa wapenzi hakuweza kupata mimba na kuitwa mama sababu Burna Boy hayupo imara(impotent).
Mrembo huyo amesema hayo huku akionesha pia kama kumkejeli na kumdhihaki Burna kwa tatizo hilo
Baada ya hapo Burna Boy akaibuka kumjibu ex wake huyo na amethibitisha kuwa ni kweli ana tatizo husika lakini hajali sana kwasababu kama ni pesa anazo, lakini staa huyo wa Nigeria hajaingia ndani zaidi kuelezea kama tatizo lake ni la kuzaliwa nalo au lah!
Kabla ya kulipuliwa na ex wake huyo, wiki zilizopita Burna Boy akihojiwa alisema kwasasa yupo singo, ametimiza miaka 31 ila bado hana mtoto na labda akija kujiona yupo katika nafasi nzuri anaweza kupata mtoto
Alisisitiza kwamba experience hiyo ni nzuri na pia ni mbaya kwake kwani tayari kiuchumi yupo vizuri na hana mtoto, lakini ndugu zake wakifurahia mafanikio au utajiri wake sio jambo baya pia
Kipindi cha nyuma waliwahi kuibuka kinadada kama wawili hivi wakidai wamezaa na Burna Boy na kutelekezwa hata hivyo mwenyewe hakuonesha kujali kinadada hao na kudai wanaongopa yeye hana mtoto.