Menu ›
Burudani
Fri, 24 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dada wa Staa wa Muziki #DiamondPlatnumz na mfanyabiashara Esma Platnumz ametia neno kwenye sakata linaloendelea baina ya Familia ya Mtangazaji Mojay na mzazi mwenzake Staa wa Muziki Gigy Money.
Kupitia ukurasa wa Instagram #Esma amesema kuwa kwa upande wake kama akiolewa katika Familia yenye Migogoro yeye hawezi kuingilia hata kama Mke mwenzake atakuwa anamtukana vipi na hawezi kumshawishi Mwanaume wake amzalilishe Mwanamke aliezaa nae.
Mbali na hivyo ameonesha kushangazwa na yanayoendelea baina ya Gigy Money, Mojay kwenye Mitandao ya kijamii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live