Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Emmanuel Mbasha apangua tuhuma za kuazima magari

8379 26864031 565090327169374 8993183294690426880 N 1 TZW

Mon, 28 May 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki wa Injili Bongo, Emmanuel Mbasha amejibu kuhusu tuhuma za kuazima magari ya watu kwa ajili kupiga picha ili kujionyesha katika mitandao.



Muimbaji huyo amesema tuhuma hizo hazina ukweli wowote kwani kazi zake anazozifanya zinatosha kumuingiza kipato cha kuweza kumiliki magari kadhaa.

“Hamna, mimi huwa siazimi magari, yote niliyona ni ya kwangu, ninatumia gari zangu na watu wa karibu yangu wanafahamu mimi ni mfanyabiashara, ninaimba Gospel na nina kipato cha kufanya mambo yangu yote ya unayoyaona,” Mbasha ameiambia Bongo5.

Ameongeza kuwa kwa sasa anamiliki magari mawili. Wimbo wa mwisho Mbasha kutoa ni Hallelujah ambao amemshirikisha Hondwa, wimbo huo ulitoka October 2017.

Loading...
Chanzo: bongo5.com