Watendaji Wakuu wa Mtandao wa X (zamani Twitter) ambao walifukuzwa kazi baada ya Elon Musk kuununua Mtandao huo, wamefungua Kesi ya madai wakimtaka Bosi huyo mpya kuwalipa Dola Milioni 128 (zaidi ya Tsh. Bil. 326) kwa kuwaondoa kazini kikatili
Kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya San Francisco walalamikaji wakiwa ni aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Twitter, Parang Agrawal pamoja na Watendaji wengine watatu wanaodai kuwa Elon alivunja haki za Wafanyakazi waliofukuzwa baada ya kuinunua kampuni hiyo
Taarifa zaidi zinadai hadi kufikia Mwaka 2021, Agrawal alikuwa na madai ya fidia yenye thamani ya zaidi ya takriban Tsh. Bilioni 76.5 kutoka katika kampuni hiyo.
Ikumbukwe, wakati Elon akiwaondoa kazini alisema Watendaji hao walikuwa na uzembe mkubwa na utovu wa nidhamu wa makusudi na hivyo halazimiki kuwalipa fidia yoyote