Msanii wa Hip Hop anayewakilisha Mwanza, Edu Boy amepita Sayarini (Planet Bongo) ya East Africa Radio mchana huu na kuweka wazi msiammo wake katika mchezo wa kamari kuwa hawezi kuacha kubeti.
Msanii wa Hip Hop anayewakilisha Mwanza, Edu Boy amepita Sayarini (Planet Bongo) ya East Africa Radio mchana huu na kuweka wazi msiammo wake katika mchezo wa kamari kuwa hawezi kuacha kubeti. "Kubeti ni lazima katika maisha yetu ya kila siku, sijui kwa wengine ila kwangu ni muhimu sana kubeti, nimeshazoea, kila mtu ana mawazo yake na namna yake ya kuishi, kwangu ni muhimu kubeti japo simshauri mwingine," amesema Edu Boy.