Menu ›
Burudani
Tue, 5 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jamaa mmoja ambaye alikuwa akiwazuga watu kuwa yeye ni Drake wa Marekani, ameshtukiwa na akaunti yake kufutwa kwenye mtandao wa Instagram.
Jamaa huyo alikuwa akiwaongopea watu kwa kufanya ni Drake mwenyewe kwenye klabu mbalimbali nchini Marekani akitumia jina la IzzyDrake Instagram.
Mwamba huyo baada ya kushtukiwa ameeleza kuwa watu walikuwa wakimuomba yeye atokee kwenye event zao kwa sababu Drake kumpata ni gharama.
“Walikuwa wananifuata DM, wananiomba niende kwenye shughuli zao kwa sababu hawawezi kumlipa Drake ambaye ni gharama kumpata,” alisema.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live