Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Drake na Kanye kwenye steji moja December

Screen Shot 2021 11 18 At 4 Drake na Kanye

Sun, 21 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

MARAPA wa kiwango cha Dunia, Drake na Kanye West kutoka Marekani, sasa uhusiano wao ni kizazi sana baada ya kumaliza bifu lao.

Drake na Ye wameungana tena ambapo Kanye ameposti picha akiwa na Drake nyumbani kwake huku Kitaa cha Toronto nchini Marekani.

Taarifa za ndani kabisa zinasema kuwa wamemaliza tofauti zao baada Kanye kutamani wapatane kwa muda mrefu. Drake na Kanye waliingia kwenye bifu kubwa baada ya Kanye ku-tweet karibia Tweets 25 akidiss na kumponda Drake kwa kile ambacho Kanye hakuwahi kufunguka sababu ilikuwa ni nini.

Ugomvi wao ulikua mkubwa zaidi baada ya Drake kutangaza kutoa album yake "Certified Lover Boy" siku ambayo Kanye alikua akiachia album ya Donda.

Hivi karibuni kwenye mahojiano na Noriega kupitia podcast ya Drink Champs, Kanye alisema yuko tayari kupanda kwenye steji za Verzuz kuchuana na Drake lakini aongezewe wasanii wengine wanne.

Tayari Drake na Kanye wametangaza kukutanga stejini Tarehe 9 December ndani ya ukumbi wa L.A. Coliseum jijini Los Angeles, California.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live