Menu ›
Burudani
Wed, 21 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Drake na Wizkid wameweka historia kwa pamoja kwa vile wimbo wao wa pamoja “One Dance” umefikisha streams Bilioni tatu kwenye mtandao wa Spotify.
Hivyo Drake anakuwa Rapa wa kwanza kuwa na wimbo wenye wasikilizaji zaidi ya Bilion tatu na Wizkid anakuwa Msanii wa kwanza kutoka Afrika kufikisha idadi hiyo katika mtandao huo wa Spotify .
Wimbo huo ambao uko kwenye albamu ya nne ya studio ya Drake “Views” ulilitolewa mwaka 2016 na katika mwaka huo huo uliweka historia kuwa wimbo uliosikilizwa zaidi kwani ulipata Streams zaidi ya milioni 880.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live