Mtayarishaji Mkongwe Wa Muziki Kutoka Marekani #DrDre ataungana na mastaa wengine wakubwa duniani waliopewa heshima ya kutunukiwa nyota kwenye Hollywood Walk of Fame.
Kwa mujibu wa mtandao wa Variety, #DRE atatunukiwa nyota hiyo Machi 19, mwaka huu Kutokana na mchango wake mkubwa kwenye tasnia ya muziki.
Dre Ataenda Kutunukiwa Nyota Hiyo Akiambatana Na Rafiki Yake Wa Karibu Wa Muda Mrefu Rapa #SnoopDogg.
Fahamu, Hollywood Walk of Fame ni eneo la kutembea kwa miguu kando kando ya majengo katika eneo la Hollywood ambapo nyota za watu waliofanya vyema kwenye upande wa burudani zimewekwa.
Walengwa ni wanamuziki, waigizaji, waelekezi wa filamu, watayarishaji wa muziki na filamu na makundi ya waigizaji.