Menu ›
Burudani
Sat, 10 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtayarishaji wa muziki maarufu duniani kutoka nchini Marekani DJ Khaled akiongozana na mkongwe wa masumbwi duniani pia kutoka Marekani wameenda kuhiji Makka nchini Saudi Arabia.
Kupitia ukurasa wa Instagram wa DJ Khaled amethibitisha hilo huku akisema kuwa ilikuwa ni ndoto yake kufika katika eneo hilo takatifu duniani kwa ajili ya kufanya ibada ya Hija ili aweze kumuomba Mwenyezi Mungu.
DJ Khaled ameongozana na Mike Tyson pamoja na baba mzazi wa Mike Tyson wote wakiwa kwenye nyumba hiyo ya Ibada Makka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live