Menu ›
Burudani
Thu, 11 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameweka bayana kuwa kwa sasa, amenunua helkopta yake.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram (Insta-Story) jana Agosti 10, 2022, Diamond ndio alitupia ujumbe mfupi sana akimshukuru Mungu kwa kumwezesha kununua helkopta.
"Mungu ni mwema, nimenunua helikopta leo."
Ikumbukwe, hivi karibuni Diamond alithibitisha kuwa tayari amenunua ndege binafsi (private jet) hivyo huu ni muendelezo wa kufuru anazozifanya Diamond. Mbali na hayo, Diamond pia ni msanii anayeongoza Bongo kwa kumiliki mandinga ya bei mbaya ikiwemo Rolls Royce.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live