Rapa Diddy ameamua kuukataa ujumbe unaodaiwa alimuandikia Staa wa muziki Burna Boy baada ya kushindwa kuondoka na Tuzo za GRAMMY.
Moja kati ya ujumbe uliosambaa katika mitandao ya Kijamii baada ya Burna Boy kukosa Tuzo hizo ni pamoja na ujumbe ulionekana kuwekwa katika Instastory ya Rapa Diddy ukisema kuwa Burna Boy amefeli kuchukua Tuzo kwa sababu hakumshirikisha kuandaa Album nyingine kama ilivyokuwa kwenye Twice As Tall iliyoshinda Tuzo ya GRAMMY 2021.
Mbali na hivyo, Rapa Diddy imembidi ajitokeze na kuukataa uvumi huo na kusema kuwa sio kweli
Diddy ndio alikuwa Excutive Producer wa Album ya Twice As Tall iliyofanikiwa kunyakuwa Tuzo ya GRAMMY 2021.