Menu ›
Burudani
Tue, 11 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtangazaji na chawa maarufu Bongo, Mwijaku amesema kamwe hamuombi hela Diamond bali huwa analipwa mshahara.
Mwijaku aliyasema hayo baada ya kuulizwa na Bongo Five kuhusu madai ya Baba Levo kwamba anamuomba hela Diamond ndipo akafafanua.
“Mimi simuombi hela Diamond. Diamond ananilipa mshahara wangu na ninamshukuru Mungu, ananilipa vizuri kila inapofika mwisho wa mwezi mimi ni balozi wa Wasafi BET,” alisema Mwijaku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live