Menu ›
Burudani
Wed, 28 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Muziki wa Singeli nchini Sholo Mwamba anatarajia kuachia album yake hivi karibuni na kikubwa na kizuri kuhusu album hiyo ni kuwa itakuwa na kolabo ya msanii Diamond Platnumz ambaye ni mwana Tandale mwenzi au kama wanavoitana vijana wengi “Home Boy”.
Uwepo wa Diamond Platnumz kwenye album hiyo umethibitishwa na yeye mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Instagram pale kwenye Instastory kwa ku-share video ya Sholo Mwamba na kuandika..
“MWAMBA THE ROCK....My Homeboy Brother, Love Always!, ....Inshallah Lazima Niwepo Kwenye Album Hio Mwanangu!...ANOTHER BOY FROM TANDALE” - Diamond
Chanzo: www.tanzaniaweb.live