Mujibu wa #TopChartsAfrica supastaa wa Bongo Fleva, @Diamond Platnumz, ndiye msanii wa kwanza Afrika (Sub Saharan Countries) kwa kuwa na watazamaji au wasikilizaji wengi zaidi (Streams) katika mtandao wa YouTube.
Ripoti hiyo imeonyesha Diamond ana jumla ya views bilioni 1.92, akifuatiwa na #BURNABOY mwenye jumla ya views bilioni 1.50
Ikumbukwe pia kwamba, #SIMBA anashikiria rekodi ta kuwa msanii namba moja Afrika (Sub Saharan Countries) kwa kuwa na wafuasi (Subscribers) wengi zaidi katika mtandao huo aa YouTube akiwa na jumla ya wafuasi milioni 6. 97.
Katika ripoti hiyo, ndani ya top 10 kuna wasanii saba kutoka Nigeria, wawili kutoka Tanzania ambao ni Diamond na Rayvanny aliyeshika nafasi ya 10 na mmoja kutoka Congo ambaye ni Fally Ipupa aliyeshika nafasi ya nne.